IRAN KUSHUTUMIWA NA MAREKANI KUSHAMBULIA HIFADHI YA MAFUTA SAUDIA
Marekani yasema Iran ilikuwa nyuma ya mashambulio ya hifadhi ya mafuta ya Saudia Marekani imetoa picha za setilaiti na kunukuu taarifa za ujasusi kuthibitisha madai yake kwamba Iran ilikuwa nyuma ya mashambulio dhidi ya vituo vya mafuta vya Saudia Iran inakana kuhusika na mashambulio hayo ya ndege , ambayo yalidaiwa kutekelezwa na waasi wa kiuhudhi wanaounga mkono Iran nchini Yemen. lakini maafisa wa Marekani ambao hawakutajwa majina wakizungumza na vyombo vya habari vya kimataifa nchini Marekani wamesema eneo na ukubwa wa mashambulio vinaonyesha kuwa Wahudhi hawakuhusika na mashambuli hayo. Tukio hilo lilisababisha kupungua kwa mauzo ya mafuta duniani kwa 5% na limesababisha kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo. Marekani inasema nini ? Waziri wa ulinzi wa Marekani Mike Pompeo aliilaumu Iran wikendi bila kutoa ushahidi wowote , jambo lililoichochea serikali ya Tehran kuushutumu utawala wa Washington kwa uongo. Katika ujumbe wake alioutoa kwneye mtandao wa kijami...
Comments
Post a Comment