MWILI WA MUGABE HAUZIKWI LEO TENA


Mazishi ya Mugabe: Mwili wa Mugabe hauzikwi leo tena




Mwili wa aliyekuwa rais wa kwanza wa Zimbabwe, Robert Mugabe umehifadhiwa katika eneo alilozaliwa mara baada ya watu kumuaga katika mji mkuu wa Harare.
Viongozi wa Afrika wamemsifu aliyekuwa rais wa Zimbabwe Robert Mugabe kama mpiganiaji wa Uhuru katika mazishi yake katika uwanja wa kitaifa mjini Harare.
Rais wa sasa Emmerson Mnagagwa alimtaja Mugabe kama kiongozi aliyekuwa na maono na kusema kwamba 'taifa letu linalia'.
Hatahivyo uwanja ulio na uwezo wa kubeba watu 60,000 ulikuwa na idadi ndogo ya watu.


Uchumi wa taifa hilo upo katika hali mbaya na raia wengi wa Zimbabwe waliamua kususia sherehe hiyo kutokana na ukandamizaji uliotekelezwa na uongozi wa Mugabe.
Kupanda kwa hali ya mfumuko na ukosefu wa ajira ni baadhi ya masuala ambayo yamewafanya raia wa taifa hilo kumlaumu Mugabe.

''Tunafurahia kwamba amefariki, kwa nini nihudhurie mazishi yake? sina mafuta'', alisema mkazi mmoja wa Harare akizungumza na AFP.
''hatutaki kusikia chochote kumuhusu tena. yeye ndio sababu ya matatizo yetu''.

Mazishi hayo yanafuatia mgogoro kati ya familia ya Mugabe na serikali kuhusu mahala atakapozikwa.


Sasa imekubalika kwamba atazikwa katika makaburi ya mashujaa mjini Harare, familia yake imesema.
Msemaji wa familia na mpwa wake leo Mugabe anasema kwamba hiyo itafanyika baada ya kipindi cha mwezi mmoja wakati ambapo kaburi hilo litajengwa katika makaburi hayo ya mashujaa .

Awali mipango ya mazishi hayo kufanyika siku ya Jumapili ilionekana kufutiliwa mbali.
Mugabe ambaye alikuwa na umri wa miaka 95 alipofariki wiki iliopita alikuwa akitibiwa nchini Singapore.
Viongozi wa Afrika , wa zamani na waliopo sasa waliingia katika uwanja huo kwa shangwe kubwa pamoja na viongozi waliopigania uhuru wa bara hili.
Rais Mnangagwa - mtu ambaye alimpindua Mugabe miaka miwili iliopita aliketi viti viwili karibu na mkewe Mugabe Grace.

Sifa za Mugabe kama mpiganiaji uhuru zilitolewa na kila kiongozi ambaye alisimamna kuhutubia akiwemo rais wa Kenya Uhuru kenyatta - huku wakitofautiana na maneno yaliotolewa na mwakilishi wa familia hiyo Walter Chidhakwa aliyesema kwamba ''Mugabe alikuwa na huzuni , huzuni mkubwa', Ilikuwa safari ngumu na ya kuchukiza''.
Matamashi yake yalionyesha wazi wasiwasi uliopo kati ya serikali iliopo na familia ya Mugabe.

Zaidi ya viongozi kumi wakiwemo wale wa zamani wa mataifa ya Afrika walihudhuria mazishi hayo , wakimsifu Mugabe kama kiongozi wa Afrika aliyeamua kutumikia maisha yake yote kwa raia wa Zimbabwe.
Rais Kenyatta alisisitiza kwamba matatizo ya Kiafrika yanahitaji suluhu ya kiafrika.
Baadae raia wallimzomea rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ikionekana kuwa jibu la ghasia dhidi ya wageni nchini kwake katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita.
Alitambua kelele hizo kwa kusema: " Katika wiki mbili zilizopita , sisi Waafrika Kusini tumekuwa tukikabiliwa na wakati mgumu.
Tumekuwa na vitengo vya ghasia katika baadhi ya maeneo ya Afrika Kusini...hili limesababisha kama ninavyowasikia mukisema ... vifo na majeraha miongoni mwa idadi ya watu. lakini alisisitiza sisi Waafrika wa Kusini hatupendi ghasia dhidi ya wageni"


Comments

Popular posts from this blog

KILIMO BORA CHA NYANYA NA SOKO LAKE

SOKO LA MIHOGO NA KANUNI ZAKE

SOKO LA TIKITI MAJI NA KILIMO CHAKE