VIONGOZI WA AFRICA KUAGA MWILI WA MUGABE
Rais wa sasa Emmerson Mnagagwa alimtaja Mugabe kama
kiongozi aliyekuwa na maono na kusema kwamba 'taifa letu linalia'.
Hatahivyo uwanja ulio na uwezo wa kubeba watu 60,000 ulikuwa na
robo ya idadi hiyo.
Uchumi wa taifa hilo upo katika hali mbaya na raia wengi wa
Zimbabwe waliamua kususia sherehe hiyo kutokana na ukandamizaji uliotekelezwa
na uongozi wa Mugabe.
Kupanda kwa hali ya mfumuko na ukosefu wa ajira ni
baadhi ya maswala ambayo yamewafanya raia wa taifa hilo kumlaumu Mugabe.
''Tunafurahia kwamba amefariki, kwa nini nihudhurie mazishi
yake? sina mafuta'', alisema mkaazi mmoja wa Harare akizungumza na AFP.
''hatutaki kusikia chochote kumuhusu tena. yeye ndio sababu ya matatizo yetu''.
Kulikuwa na jua , na raia wachache
waliokuwepo kumpatia mkono wa burihani Robert Mugabe.
Wakati ambapo jeneza ambalo lilikiuwa
likimbeba mwanzilishi wa taifa hilo lilipoingia uwanjani ilikuwa wazi kwamba ni
idadi ndogo walihudhuria sherehe hiyo ya mazishi.
Viongozi wa Afrika , wa zamani na
waliopo sasa waliingia katika uwanja huo kwa shangwe kubwa pamoja na viongozi
waliopigania uhuru wa bara hili.
Bwana Mnangagwa - mtu ambaye
alimpindua Mugabe miaka miwili iliopita aliketi viti viwili karibu na mkewe
Mugabe Grace.
Sifa za Mugabe kama mpiganiaji uhuru
zilitolewa na kila kiongozi ambaye alisimamna kuhutubia akiwemo rais wa Kenya
Uhuru kenyatta - huku wakitofautiana na maneno yaliotolewa na mwakilishi wa
familia hiyo Walter Chidhakwa aliyesema kwamba ''Mugabe alikuwa na huzuni ,
huzuni mkubwa', Ilikuwa safari ngumu na ya kuchukiza''.
Matamashi yake yalionyesha wazi
wasiwasi uliopo kati ya serikali iliopo na familia ya Mugabe.

Zaidi ya viongozi kumi wakiwemo wale
wa zamani wa mataifa ya Afrika walihudhuria mazishi hayo , wakimsifu Mugabe
kama kiongozi wa Afrika aliyeamua kutumikia maisha yake yote kwa raia wa
Zimbabwe.
Bwana Kenyatta hakusita katika
matamshi yake aliposema kwamba matatizo ya Kiafrika yanahitaji suluhu ya
kiafrika.
Baadaye raia wallimzomea rais wa
Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ikionekana kuwa jibu la ghasia dhidi ya wageni
nchini mwake katika kipindi cha mwezi mmoja uliokwisha.
Alitambua kelele hizo kwa kusema: Katika
wiki mbili zilizopita , sisi Waafrika Kusini tumekuwa tukikabiliwa na wakati
mgumu .
Tumekuwa na vitengo vya ghasia katika
baadhi ya maeneo ya Afrika Kusini...hili limesababisha kama ninavyowasikia
mukisema ... vifo na majeraha miongoni mwa idadi ya watu. lakini alisisitiza
sisi Waafrika wa Kusini hatupendi ghasia dhidi ya wageni
Je Mugabe atazikwa wapi?
Mazishi hayo yanafuatia mgogoro kati
ya familia ya Mugabe na serikali kuhusu mahala atakapozikwa.
Sasa imekubalika kwamba atazikwa
katika makaburi ya mashujaa mjini Harare, familia yake imesema.
Msemaji wa familia na mpwa wake leo
Mugabe anasema kwamba hiyo itafanyika baada ya kipindi cha mwezi mmoja wakati
ambapo kaburi hilo litajengwa katika makaburi hayo ya mashujaa .
Awali mipango ya mazishi hayo kufanyika siku ya
Jumapili ilionekana kufutiliwa mbali.
Mugabe ambaye alikuwa na umri wa miaka 95 alipofariki wiki
iliopita alikuwa akitibiwa nchini Singapore
Mwaka 1982 aliushutumu upinzani kwa kujaribu kupindua serikali
Maelfu ya watu waliuawa alipolituma jeshi lake lililopata
mafunzo Korea Kaskizini, kuwakandamiza maadui zake
Mwaka 1987,alibadilisha katiba ili imruhusu kuwa rais na
kuongeza mamlaka yake
Uchumi ulidororeka baada ya mwaka 2000…
Wakati Mugabe aliagiza kunyakua mashamba yaliomilikiwa na watu
weupe yaliyokuwa kinara ya uchumi
Mfumuko wa bei ulipelekea sarufi ya taifa kuwa bila thamani na
hali nchini humo ikazidi kudororeka
Baada ya uchaguzi wa mwaka 2008, Mugabe alilazimika kugawanya
mamlaka na kiongozi wa upinzani Morgan Tsvangirai
Japo kulikuwa na ghasia dhidi ya wafuasi wa Bw Tsvangirai katika
kampeni za uchaguzi
Ndoa yake na Grace Mugabe ,anayemzidi kwa maika 40, yaweza kuwa
iliyomponza
Wengi walikasirishwa na Grace kuandaliwa kuwa mrithi wake.
Comments
Post a Comment