Posts

Showing posts with the label teknology

YOUTUBE WITH FAKE VIDEOS

Image
Matangazo ya uongo ya video za matibabu ya saratani kunufaisha mtandao wa Youtube Uchunguzi uliofanywa na BBC, umebaini kuwa kuna video za lugha mbalimbali katika chaneli za Youtube, zinazotoa taarifa ambazo sio sahihi za matibabu ya saratani. Na matangazo mengine yanayoongoza kwa taarifa za uongo ni video za bidhaa mbalimbali na vyuo vikuu. Katika lugha 10 zilizopo Youtube, BBC ilibaini zaidi ya video 80 ambazo zina maudhui ya afya ambayo sio sahihi haswa ya ugongwa wa saratani. Katika video 10 zilizochunguzwa tayari watu zaidi ya milioni wameangalia. Wengi walivutiwa na matangazo hayo. Tiba ambazo hazijathibitishwa ambazo zinadai kuwa vitu kama ukwaju au amira kuwa tiba. Juisi au kufunga ni miongoni mwa tiba zilizokuwa zinafundishwa katika video hizo. Watumiaji wengine wanahamasisha watu kunywa maziwa ya Punda huku wengine wakitaka watu wanywe maji ya moto. Huku hakuna hata tiba yeyote kati walizotaja imethibitishwa kitaaluma kuwa inatibu saratani. Inaonek...

APPLE NA IPHONE 11,PRO NA PRO MAX

Image
Kwa Apple tarehe 10 Septemba 2019 ilikuwa ni siku ya kutambulisha simu zao mpya – iPhone 11, ila sehemu kubwa ya utambulisho huo ulihusisha zaidi huduma zake zingine mbalimbali. Katika tukio hilo lilifanyika katika makao makuu ya kampuni hiyo Cupertino, Apple walitambulisha kwa undani huduma zao za Apple TV, iPad, iPhone 11, mfumo wa magemu wa Apple Arcade, na saa mpya ya Apple Watch Series 3. Saa ya Apple Watch Series 3 Wametambulisha toleo jipya la saa ya Apple Watch Series 3. Kikubwa hapa ni kwamba saa hizo zimepunguzwa bei kutoka dola 279 (zaidi ya Tsh 600,000/=) na sasa toleo hili jipya litapatikana kwa dola 200 tuu (takribani Tsh 430,000/=) Huduma ya Apple TV+ Huduma ya kutazama vipindi kwa mfumo wa mtandao, mpinzani wa huduma ya Netflix, Apple TV+ itaanza kupatikana Novemba na itagharimu dola 4.99 kwa mwezi (Takribani Tsh 11,000/=) iPad mpya ni takribani Tsh 700,000 Pia Apple wametambulisha iPad mpya ya ukubwa wa display wa inchi 10.2. Wameo...

GOOGLE YAPIGWA FAINI NA UFARANSA YA $1 BILLION

Image
Wakati Marekani na Ufaransa wakifanya mazungumzo juu ya suala la kodi kwa makampuni ya biashara za kimtandaoni hasa hasa ya kimarekani tayari taarifa imetoka inayosema Google wamepigwa moja ya faini kubwa zaidi kuwahi kutolewa huko nchini Ufaransa. Ni miezi sasa tokea serikali ya Marekani ipandishe kiwango cha kodi dhidi ya vinywaji vya divai (wine) vya nchini Ufaransa vinavyoingizwa Marekani, uamuzi huo ulikuja baada ya serikali ya Ufaransa kudai ya kwamba inataka kudai kodi nyingi kutoka kwa makampuni ya biashara za kimtandao kama Google, Facebook, Amazon na mengineyo. Suala hilo halikupendwa Marekani kwa kuwa makampuni haya mengi ni ya nchini humo na huwa wanatoa ripoti zao za kifedha na kulipa kodi nchini Marekani na hivyo uamuzi wa Ufaransa unaweza kuwa kandamizi na kupunguza kodi kwa Marekani. Wakati tayari serikali hizo mbili zimesema zitafanya mazungumzo kuhusu jambo hilo wachunguzi wa masuala ya kodi nchini Ufaransa wamefanikiwa kufikia makubaliano na Goo...

FACEBOOK WANAJUA WATUMIAJE WAKE WANAPOFANYA NGONO

Image
  Facebook wanafahamu ‘watumiaji’ wake wanapofanya ngono Je unaweza unaweza kufikiri ni vigumu Facebook kufahamu pale watumiaji wake wanapofanya ngono? Imefahamika si vigumu, na yote yanafanikishwa kupitia mifumo ya data za apps na huduma za matangazo ya  Facebook . Shirika linalotetea haki za watu dhidi ya teknolojia za kisasa – Privacy International limetoa ripoti inayoonesha tovuti maarufu ya mtandao wa kijamii ya Facebook kwamba huwa unataka kufahamu hadi maisha ya kingono ya watumiaji wake ili kutumia data hizo kwenye huduma zake za kimatangazo. Apps za uzazi na kufuatilia mizunguko ya hedhi ni maarufu sana hasa hasa kwa wanawake. Ripoti ya Privacy International inaonesha kupitia teknolojia zake za kimatangazo za Facebook zinazowekwa kwenye apps hizo baadhi ya apps maarufu zimekuwa zikituma (kushare) taarifa za watumiaji wake na hali zao hii ikiwa ni pamoja na masuala ya ngono kwenda huduma ya matangazo na data ya Facebook. Apps za masuala ya uzazi na ...

UBER KUJA KIUSALAMA ZAIDI

Image
Kampuni ya Uber inatarajia kuzindua sasisho lake jipya ambalo litamwezesha mteja kusafiri kwa usalama zaidi nyakati za usiku bila wasi. Toleo Hili litakuwa linafanyakazi kwa njia hii hapa, Kuna muda unaweza ukawa umeagiza usafiri ukufate Ila matokeo yake unajikuta umeingia katika gari ambalo silo, Sasa ili kuepusha visanga hivyo, Uber inaleta kitu kipya ambacho kinaitwa Pin, yaani kabla ya kuingia kwenye gari uliloagiza likufate, unamtumia dereva pincodes, dereva zikimfikia B asi wewe utapokea Ujumbe kwamba Hilo ndilo gari uliloagiza Ila Kama Ujumbe hautofika kwako Hilo si gari lenyewe. Toleo hili linatarajiwa kuanza kufanyakazi majira ya usiku tu

INSTAGRAM KUUA SOKO LA TIK TOK

Image
Wakati mtandao wa Snapchat ulipokuwa unatrend na staili take ya posti zinazodumu kwa masaa 24, Instagram waliamua kuja na staili Kama hiyo ili kuwapoteza katika ramani kwa kuanzisha kitu kinachoitwa "stories". Sasa Instagram inakuja na kitu kingine kipya kinachoitwa "Clips", hiki kitakuwa kinafanyakazi kama mtandao wa Tiktok, kwa ambao hamfahamu mtandao wa Tiktok, ni moja ya mitandao ambayo inakuja Sana kwa Kasi, kwa maujanja ya video zikiwa na effect zenye ujazo wa juu. Inst agram Clips itakuwa na uwezo wa mtu kuposti video zikiwa na ujazo wa filters na effect ambazo zitaufanya mtandao huu kuzidi kupata umaarufu mwingi zaidi.

MICROSOFT IMETULETEA "YOUR PHONE"

Image
kampuni ya Microsoft inajaribu kuwasogeza watumiaji wengi kuwa karibu na windows 10 kwa kuleta toleo la "Your Phone" ambalo mtumiaji was Windows 10 ataweza kuionganisha simu take na PC take na kuweza kutuma na kupokea sms bila ya kugusa simu yako. Sasa good news ni kwamba, Microsoft wameupdate toleo hili na kulifanya kuwa la kitofauti kabisa baada ya kuongeza na Huduma ya kuweza kupiga nakupokea simu moja kwa moja ukiwa na PC yako, Yaani hutakuwa na haja ya kushika simu yako kumpigia mtu, vyote utakuwa unamaliza kwenye PC yako. x